Author: Sukuma legacy

1213. GWIWILA GULIHO UGWIYIGWA NDUHU.

Bhaliho bhanhu bha ha kaya ndebhe abho bhilomelaga higulya ya kutumama milimo yabho. Aliyo lulu, umuwilomeji bhobho bhunubho abhanhu bhenabho, bhalidiigwagwa chiza, kunguno ya gukija gwidegeleka chiza umumahoya gabho genayo. Abhoyi bhayoganyaga ulu bhaliyomba kunguno ya bhuli ng’wene guhaya adegelekwe wei duhu. Hunagwene bhagayomba giki, “gwiwila guliho ugwiyigwa nduhu.”

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagapangaga chiza imilimo ya gutumama aha kaya yabho, aliyo ugutimija nduhu. Abhanhu bhenabho bhagilomelaga higulya ya kutumama nimo nnebhe bhiyigwa chiza, aliyo lulu ulu lyushiga ilikanza lya gugumama unimo gunuyo, bhuli ng’wene agajaga kunimo gokwe duhu, umuwikaji bhobho. Abhoyi bhagadumaga kujibheja chiza ikaya jabho jinijo, kunguno ya kuleka uguitimija imilimo iyo bhagayipangaga guyitumama, aha kaya jabho jinijo.

Abhanhu bhenabho, bhagikolaga nabho bhahoyaga bhiigwa bho nduhu ugwidegeleka chiza, kunguno nabhoyi bhapangaga milimo yao bho mihayo aliyo uguitimiza nduhu aha kaya yabho yiniyo. Hunagwene bhagayombaga giki, “gwiwila guliho ugwiyigwa nduhu.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gubhiza na ng’wigwano gogujilanija chiza, umubhupangi bho milimo yabho kihamo na guyitumama chiza, kugiki bhadule gujibheja chiza ikaya jabho, umuwikaji bhobho.

Luka 11:23.

Luka 11:27-28.

Luka 15:9-10.

Marko 14:17-21.

Yohana 15:1-3.

KISWAHILI: KUAMBIANA KUPO KUELEWANA HAKUNA.

Walikuwepo watu kwenye familia fulani waliokuwa katika maongezi yao juu ya kufanya kazi zao. Lakini katika maongezi hayo watu hao walikuwa hawaelewani vizuri, kwa sababu ya kutosikilizana vizuri katika maongezi hayo. Wao walikuwa wakipiga kelele katika kuongea kwao kwa sababu ya kila mmoja wao kutaka asikilizwe yeye tu. Ndiyo maana walisema kwamba, “kuambiana kupo kuelewana hakuna.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa watu wanaopanga vizuri kazi za kufanya bila kuzitekeleza, kwenye familia yao. Watu hao huongea juu ya kufanya kazi fulani na kuelewana vizuri, lakini ukifika wakati wa kuifanya kazi hiyo, kila mmoja huenda kwenye kazi yake tu, maishani mwao. Wao hushindwa kuziendeleza vizuri familia zao hizo, kwa sababu ya kuacha kuzitekeleza kazi zao walizozipanga, katika familia zao hizo.

Watu hao, hufanana na wale waliopanga kufanya kazi zao vizuri, bila kuzitekeleza, kwa sababu nao hupanga kazi za kufanya vizuri bila kuzitimiza, kwenye familia zao hizo. Ndiyo maana wao husema kwamba, “kuambiana kupo kuelewana hakuna.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuwa na uelewano wa kushirikiana vizuri katika kupanga kazi zao na kuzitekeleza kwa pamoja, ili waweze kuziendeleza vizuri familia zao, maishani mwao.

Luka 11:23.

Luka 11:27-28.

Luka 15:9-10.

Marko 14:17-21.

Yohana 15:1-3.

ENGLISH: TALKING TO EACH OTHER WHERE THERE IS NO MUTUAL UNDERSTANDING.

There were people in a family who were talking about doing their jobs. But in their conversations, they did not understand each other well, because of not listening well to each other while talking. They were shouting in their speech because each of them wanted to be listened by others. That is why they said that, “talking to each other where there is no mutual understanding.”

This saying is related to people who plan well the tasks to be done without carrying them out, in their family. Those people talk about doing some works and get along well, but when a time of doing them comes, everyone just goes to his/her works, in their lives. They fail to develop their families well, because of stopping to carry out their planned tasks, in their lives.

Those people are similar to those who planned to do their jobs well, without carrying them out, because they also plan jobs to do well without fulfilling them, in their families. That is why they say that, “talking to each other where there is no mutual understanding.”

This saying teaches people about having an understanding that is good enough to cooperate well in planning their works and carrying them out together, so that they can develop their families well, in their lives.

Luke 11:23.

Luke 11:27-28.

Luke 15:9-10.

Mark 14:17-21.

John 15:1-3.

women-6886782_1280

1212. MBEHO YA NANHA IDUNHANGIJA MUNHU NA LIMI.

Imbuki ya kahayile kenako, ilolile bhudoni bho nanha. Unanha kali kanti kadoo aka kadadulile gubheja mbeho ya gudula gunhangija munhu gupya limi. Unanha gunuyo gugatemagwa na kubhejiwa chiza kulonguno ya gwidimilija na kutumamila milimo yingi iyo ikolile na gunuyo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “mbeho ya nanha idunhangija munhu gupya limi.”

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agisagilagwa ginhu jigehu bho gujiganikila giki, jidulile gung’wambilija hatale, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agilendejaga nulu gutumama milimo yakwe ya gulima iyo idulile gung’wambilija hatale, kunguno ya gusendamila hamo ginhu jidoo guti igunila limo duhu lya mandege, aha kaya yakwe. Uweyi apandikaga makoye ga gugaiwa ijilwa aha kaya yakwe ulu ujimala ijo alijo jinijo, kunguno ya kuleka gwichobhela jikolo ja gudula gung’wambilija hatale, umuwikaji bhokwe bhunubho.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agiiganikilaga imbeho ya nanha giki idadulile gunkinga gupya limi, kunguno nuweyi agisagilagwa ginhu jigehu ulu ujipandika bho kuleka gutumama milimo ya gudula gung’wenhela sabho ja gung’wambilija hatale aha kaya yakwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “mbeho ya nanha idunhangija munhu gupya limi.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya kuleka gujisagiilwa jikolo jigehu bho guleka gutumama milimo yabho, kugiki bhadule gwikomeja kuitumama chiza imilimo yabho iya gubhambilija hatale ugujibheja chiza ikaya jabho.

Mwanzo 18:5.

I Wafalme 17:10-16.

KISWAHILI: KIVULI CHA FIMBO HAKIMZUII MTU KUCHOMWA NA JUA.

Chanzo cha msemo huo chaangalia udogo wa fimbo. Fimbo ni mti mdogo na mwembamba usioweza kutengeneza kivuli cha kuweza kumzuia mtu asichomwe na jua. Fimbo hiyo hutengenezwa kwa lengo la kujishikilia na kwa matumizi mengine yanayofanana na hilo. Ndiyo maana watu husema kwamba “kivuli cha fimbo hakimzuii mtu kuchomwa na jua.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hutegemea kitu kidogo kwa kukifikiria kwamba kitaweza kumsaidia pakubwa, katika maisha yake. Mtu huyo, hujisahau kiasi cha kuchelewa hata kufanya kazi mbalimbali zikiwemo zile za kulima, baada ya kupata kitu kidogo akitumainia kuwa kitaweza kumsaidia pakubwa, badala ya kujibidisha kukiongeza, katika familia yake. Yeye hukumbwa na matatizo mbalimbali yakiwemo yale ya kukosa chakula katika familia yake hiyo, baada ya kukimalia kile alichokuwa akikitegemea, kwa sababu ya kuacha kujitafutia mahitaji yatakayoweza kumsaidia pakubwa, maishani mwake.

Mtu huyo, hufanana na yule anayekifikiria kivuli cha fimbo kama kitaweza kumzuia kuchomwa na Jua, kwa sababu naye hutegemea kitu kidogo kwa kukifikiria kuwa kitaweza kumsaidia pakubwa, mpaka anaishiwa chakula katika familia yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “kivuli cha fimbo hakimzuii mtu kuchomwa na jua.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuacha tabia ya kutegemea kusaidiwa pakubwa na kitu kidogo, ili waweze kujibidisha kufanya kazi za kuwaletea mafanikio makubwa katika familia zao.

Mwanzo 18:5.

I Wafalme 17:10-16.

ENGLISH: THE SHADOW OF A STICK DOES NOT PREVENT A PERSON FROM BEING BURNED BY THE SUN.

The origin of this saying looks at the smallness of the stick. A stick is a small and thin tree that cannot create a shade that can prevent a person from getting sunburned. This rod is made for the purpose of holding oneself and for other similar uses. That is why people say that “the shadow of a stick does not prevent a person from being burned by the Sun.”

This saying is equaled to a person who depends on something which is small thinking that it would be able to help him a lot in his life. Such person forgets himself so much that he even does various tasks including farming, after finding something small, hoping that it will be able to help him a lot, instead of increasing it, in his family. He suffers from various problems, such as lack of food in his family, after finishing what he was relying on, because he stopped looking for the needs that will help him a lot, in his life.

This person resembles the one who thinks of the shadow of a stick as being able to prevent him from being burned by the Sun, because he also depends on a small thing thinking that it would be able to help him a lot, until he runs out of food in his family. That is why people tell him that, “the shadow of a stick does not prevent a person from being burned by the Sun.”

This saying imparts in people an idea of stopping relying on a lot of help from little things, so that they can work hard enough to bring them great success in their families.

Genesis 18:5.

I Kings 17:10-16.

stick-fight-412666_1280

 

 

 

 

1211. NDUHU UYO WIMANILE INTONDO.

Aho kale olihoyi munhu uyo owilagwa aje gujutumama milimo yakwe ohaya giki, aguja ntondo. Umunhu ng’wunuyo, agikala adalimile ungunda mpaga nose jushila ijidiku, kunguno ya gumana wiganika giki aguja ntondo aliyo adaimanile intondo yiniyo. Hunagwene abhanhu bhagang’wila giki, “nduhu uyo wimanile intondo.”

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo alingokolo ugutumama imilimo ya aha kaya yakwe, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agapangaga uguja ukumilimo bho mihayo duhu ulu lwashika ilikanza lya gutumama, okija, kunguno ya bhugokolo bhokwe, umuwikaji bhokwe. Uweyi agikalaga ukoya na nzala ya gugaiwa jiliwa aha kaya yakwe kunguno ya bhugokolo bhokwe ubho guleka gutumama milimo, umuwikaji bhokwe bhunubho.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo owilagwa aje agatumamile milimo yahaya giki aguja ntondo, mpaga nose jushila ijidiku, kunguno nuweyi agapangaga kuja kujutumama milimo okija, kunguno ya bhugokolo bhokwe, mpaga nose ogaiwa ijiliwa aha kaya yakwe, ukukikalile kakwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “nduhu uyo wimanile intondo.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya kuleka bhugokolo bho gutumama milimo kugiki bhadule gwigulambija kuitumama chiza imilimo ya gubhapandikila sabho ja gutumila umukaya jabho.

Mathayo 6:32.

Yakobo 4:14.

Luka 12:29.

KISWAHILI: HAKUNA AIJUAYE KESHO.

Hapo zamani alikuwepo mtu mmoja aliyekuwa akiambiwa na watu aende kufanya kazi, na kuwajibu watu hao kwamba, atatenda kesho. Mtu huyo, aliishi bila kulima shamba mpaka mwishowe kipindi cha masika kikapita, kwa sababu ya kufikiria kwamba ataenda kesho bila kuelewa kwamba, hiyo kesho haijui. Ndiyo maana watu walimwambia kwamba, “hakuna aijuaye kesho.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ni mvivu wa kufanya kazi kwenye familia yake, katika maisha yake. Mtu huyo, hupanga kwenda kufanya kazi kwa maneno tu, ukifika huo wakati, huacha kutekeleza, kwa sababu ya uvivu wake wa kufanya kazi maishani mwake. Yeye huhangaishwa na tatizo la njaa ya kukosa chakula kwenye familia yake kwa sababu ya uvivu wake wa kutofanya kazi, katika maisha yake.

Mtu huyo, hufanana na yule alieambiwa kwenda kufanya kazi apapanga kwenda kesho, bila kutekeleza mwishowe kipindi cha masika kikaisha, kwa sababu naye hupanga kwenda kufanya kazi bila kutekeleza mpaka anakumbwa na tatizo la njaa ya kukosa chakula katika familia yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “hakuna aijuaye kesho.”

Msemo huo hufundisha watu juu ya kuacha uvivu wa kufanya kazi kwa kujibidisha kuyatekeleza majukumu ya kuwapatia mali za kutumia katika familia zao, ili waweze kujipatia maendeleo, maishani mwao.

Mathayo 6:32.

Yakobo 4:14.

Luka 12:29.

ENGLISH: NO ONE KNOWS TOMORROW.

Once upon a time there was a man who was being told by people to go to work, and he replied to them saying “I will go tomorrow.” Such person lived without cultivating the field until the spring period was over, because of thinking that he would go tomorrow without understanding that, there is no one who knows the tomorrow. That is why people told him that, “no one knows tomorrow.”

This saying is related to a person who is lazy to work on his family, in his life. Such person plans to go to work only in words, when the time comes, he stops implementing it, because of his laziness in his life. He was worried about the problem of hunger and lack of food in his family because of his laziness of not working, in his life.

This person is similar to the one who was told to go to work without going by planning that he would go tomorrow until the spring period was over, because he also plans to go to work without carrying out until he is faced with problems of hunger and lack of food in his family. That is why people tell him that, “no one knows tomorrow.”

This saying teaches people about stopping working lazily by forcing themselves to fulfill their responsibilities which can provide them with enough assets to use in their families, so that they can make progress in their lives.

Matthew 6:32.

James 4:14.

Luke 12:29.

motorcycle-7221472_1280

1210. LWINZI LWISE LO MASHISHIWE.

Amashishiwe gali mageleshi ayo gagikalaga madamu guti mawe. Bhalihoyi bhanhu abho bhakumbaga lwinzi umuchalo jilebhe. Abhanhu bhenabho bhagalipunila ligeleshi ilo lyalilidimu guti liwe. Abhoyi bhagigulambija gukumba bho gutumila masala gabho chiza mpaga nose bhugapandika maminzi ayo bhagasholaga. Hunagwene bhagayomba giki, “Lwinzi lwise lo mashishiwe.”

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agigulambijaga gutumama milimo midimu bho gutumila masala gakwe chiza mpaga uyimala chiza, umubhutumami bhokwe. Umunhu ng’wunuyo, agatumama milimo yakwe bho gwiganika chiza na wiyumilija bhutale kunnguno ya bhukamu bhowe ubho gutumama milimo bhunubho, umuwikaji bhokwe. Uweyi agapandikaga sabho ningi noyi aha kaya yakwe kunguno ya bhukamu bhokwe ubho gutumama milimo yakwe chiza chiniko, aha kaya yakwe yiniyo.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nabho bhagigulambija gukumba lwinzi lo ha mageleshi mpaga bhuduja ugupandika aminzi, kunguno nuweyi agigulambijaga gutumama milimo midimu bho gutumila masala mingi mpaga oyimala chiza, umubhutumami bhokwe bhunubho. Hunagwene agayombaga giki, “Lwinzi lwise lo mashishiwe.”

Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya gwigulambija gutumama milimo yabho bho gutumila masala chiza mpaga bhayimala chiza, kugiki bhadule gupandika sabho ningi, umukaya jabho.

Kutoka 3:7-10.

Mwanzo 11:1-8.

KISWAHILI: KISIMA CHETU KINA MIAMBA.

Miamba hiyo ni aina ya mawe yenye ugumu wa kuweza kuvunjika kiraisi yanapogongwa kwa nguvu. Walikuwepo watu waliokuwa wakichimba kisima kwenye kijiji fulani. Watu hao, walikumbana na aina hiyo ya mawe yaliyowapatia ugumu katika kuchimba. Wao walijibidisha kuchimba kwa kutumia akili zao vizuri mpaka mwishowe wakayapata maji waliokuwa wakiyatafuta. Ndiyo maana walisema kwamba, “kisima chetu kina miamba.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hujibidisha kufanya kazi ngumu kwa kutumia akili zake vizuri mpaka anazimaliza, katika utekelezaji wa kazi zake. Mtu huyo, huzitekeleza kazi zake kwa kufikiri vizuri na kwa uvumilivu mkubwa mpaka anazimaliza, kwa sababu ya bidii yake hiyo ya kufanya kazi, maishani mwake. Yeye hupata mafanikio ya kuwa na mali nyingi sana kwenye familia yake, kwa sababu ya bidii yake hiyo ya kufanya kazi vizuri, katika maisha yake.

Mtu huyo, hufanana na wale waliojibidisha kuchimba kisima chenye miamba mpaka wakayapa maji, kwa sababu naye hujibidisha kufanya kazi ngumu mpaka anazimaliza vizuri, katika kazi zake. Ndiyo maana husema kwamba, “kisima chetu kina miamba.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kujibidisha kufanya kazi zao kwa kutumia akili zao vizuri, mpaka wanazikamilisha vizuri, ili waweze kupata mafanikio ya kuwa na mali nyingi, katika familia zao.

Kutoka 3:7-10.

Mwanzo 11:1-8.

ENGLISH: OUR WELL HAS ROCKS.

Rocks are types of hard stones which are hard to break when someone hits them. There were people who were digging a well in a certain village. Those people encountered those kinds of stones which made their work difficult for them to dig. They had to dig by using their minds well until they finally found some water which they were looking for. That is why they said that, “our well has rocks.”

This saying is equated to a person who tries to do hard works by using his mind well until he finishes them, in fulfilling his responsibilities. Such person carries out his tasks by thinking well and with great patience until he finishes them, because of his hard working situation in his life. He achieves success of having a lot of wealth in his family, because of his hard working life.

This person resembles to those who had to dig a well with rocks until they got some water, because he also does hard works until he finishes them well, in his works. That is why he says that, “our well has rocks.”

This saying teaches people about working hard enough to finish their jobs by using their minds well, so that they can get successes of having a lot of wealth, in their families.

Exodus 3:7-10.

Genesis 11:1-8.

people-6556791_1280

 

 

 

1209. KALAGU –  KIZE. NANHA GWA NTEMI GUDANHAGWA NGI – MBULA.

Imbuki ya kalagu yiniyo ilolile mbula kunguno ulu giki ilitula amamoto yayo gagizaga gagololokile gwinga ng’wigulya. Agoyi gagabhizaga magololoku ugwiza ahasi giti namha gwa Ntemi uyo nulu ngi idadulile ugudanha. Giko ulu ingi idadulule ugudanha ahigulya ya mamoto ga mbula yiniyo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “nanha gwa mtemi gudapanhagwa ngi – mbula.”

Ikalagu yiniyo, igalenganijiyagwa kuli munhu uyo alinikujo ukujikolo ijabhatale bhakwe, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agajitumamilaga bho likuja litale ijikolo ija bhatale bhakwe bhunabho, kunguno ya lilange lwakwe ilyawiza, umuwikaji bhokwe. Uweyi agabhelelaga abhanhu bhakwe bho gwikala bhikujije chiza aha kaya yakwe kunguno ya nhungwa jakwe ijawiza jinijo, umuwikaji bhokwe bhunubho.

Umunhu ng’wunuyo agikikolaga na mamoto agambula ayo gadanhagwa ngi, kunguno nuweyi agajitumamila bho likujo litale ijikolo ija bhatale bhakwe bhenabho, aha kaya yakwe. Hunagwene agabhawilaga abhanhu giki, “nanha gwa Ngemi gudadanhagwa Ingi – Mbula.”

Ikalagu yiniyo, yalanga bhanhu higulya ya gujitumila ijikolo ijabhatale bhabho bho likujo litale, kugiki bhadule kupandika mbango ja kujibheja chiza ikaya jabho, umuwikaji bhobho.

1Petro 2:17.

Warumi 12:10.

Warumi 13:7.

KISWAHILI: KITENDAWILI – TEGA.

FIMBO YA MTEMI HAIKANYAGWI NA NZI – MVUA.

Chanzo cha kitendawili hicho chaangalia mvua kwa sababu matone ya mvua hiyo huja yakiwa yamenyoka kutoka juu wakati yanaposhuka. Yenyewe huwa yamenyoka kama fimbo ya Mfalme kiasi cha kushindwa kutua hata Inzi. Yenyewe hushuka yakiwa yamenyoka mpaga kufikia hali ya Inzi kutoweka kutua pale. Hivyo basi, Inzi hawezi kutua kwenye matone hayo ya mvua. Ndiyo maana watu huhadishiana kwa kusema kwamba, “Fimbo ya Mtemi haikanyagwi na Inzi – mvua.”

Kitendawili hicho, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ana heshima kwenye vitu vya wakubwa wake, katika maisha yake. Mtu huyo, huvifanyia kazi vitu vya wakubwa wake hao kwa heshima kubwa kwa sababu ya malezi yake mema, maishani mwake. Yeye hufanikiwa kuwalea vyema watu walioko kwenye familia yake kwa sababu ya malezi yake mema aliyojifunza, katika maisha yake.

Mtu huyo, hufanana na matone ya mvua ambayo hayakanyagwi na Inzi, kwa sababu naye huvifanyia kazi vitu vya wakubwa wake kwa heshima kubwa, katika familia yake. Ndiyo maana huwaambia watu kwamba, “Fimbo ya Mtemi haikanyagwi na Inzi – mvua.”

Kitendawili hicho, hufundisha watu juu ya kutuvitumia kwa heshima vitu wa wakubwa wao, ili waweze kupata Baraka za kuzilea vyema familia zao, maishani mwao.

1Petro 2:17.

Warumi 12:10.

Warumi 13:7.

ENGLISH: I HAVE A RIDDLE – LET IT COME.

THE KING’S ROD IS NOT TRAMPLED BY FLIES – RAIN.

The overhead riddle looks at the rain because its raindrops come from above as they fall. It is often twisted like a King’s rod to the extent that even a fly cannot land on it. It descends as if it were a snake to reach the status of a fly disappearing to land there. Therefore, the fly cannot land on those raindrops. That is why people argue with each other by saying, “The king’s rod is not trampled by flies – rain.”

This riddle is related to a person who has respect for belongings of his elders, in his life. Such person works for the possessions of his superiors with great respect because of his good upbringing, in his life. He succeeds in raising the people in his family well because of his good education he learned in his life.

This person is like raindrops that are not trampled by flies, because he works for the things of his superiors with great respect, in his family. That is why they tell people that, “The king’s rod is not trampled by flies – rain.”

This riddle imparts in people an idea of using their elders’ things with respect, so that they can get blessings of raising their families well, in their lives.

1 Peter 2:17.

Romans 12:10.

Romans 13:7.

 

 

rain-5630234_1280