Yalihoyi nzuki iyo yaliyabisija bhuki gete mpaka nose bhuyutinika gufumila umumalela gabho mpaga bhoshiga hasi. Aho bhayibhona abhanhu bhagatogwa mpaka bhupanga lushigu lo guja gujiyapila. Hunagwene bhagayomba giki, “inzuki yeniyi hi ilina nzwezwe.”
Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agaidililaga chiza imilimo jakwe mpaga oimala chiza umubhutumami bhokwe. Umunhu ng’wunuyo agalimaga migunda mitale iyo agayilimililaga ngese mpaga oyimala kunguno ya bhudiliji bhokwe bhunubho umumilimo yakwe. Uweyi agabishaga majiliwa mingi noyi aha kaya yakwe kunguno ya bhukamu bhokwe ubho gutumama milimo yakwe chiza bhunubho, umuwikaji bhokwe.
Umunhu ng’wunuyo agikolaga ni nzuki iyo yaliyabisija bhuki wingi gete, kunguno nuweyi agalimaga migunda ojidilila chiza mpaga opandika sabho ningi gete, umubhutumami bhokwe bhunubho. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “inzuki yiniyi hi ilina nzwezwe.”
Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya guidilila chiza imilimo yabho bho guitumama mpaga bhapandike sabho ningi, kugiki bhadule gujilanhana chiza ikaya jabho, umuwikaji bhobho bhunubho.
Yohana 15:1-2.
Yoshua Bin Sira 11:3.
KISWAHILI: NYIKI HAWA WANA ASALI.
Walikuwepo nyuki waliokuwa wameivisha asali sana mpaka ikaanza kudondoka chini kutoka kwenye masega yake. Watu walipoona hivyo walifurahi na kupanga muda ya kwenda kulina asali hiyo. Ndiyo maana walisema kwamba, “nyuki hawa wana asali.”
Msemo huo hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huijali vizuri kazi yake mpaka anapata mafanikio mengi, katika maisha yake. Mtu huyo, hulima mashamba makubwa ambayo huyatunza kwa kuyapalilia palizi vizuri mpaka anavuna mazao kwa sababu ya kujali kwake vizuri kazi zake, katika utekelezaji wa majukumu yake. Yeye hupata mavuno mengi sana kwenye familia yake kwa sababu ya bidii yake hiyo ya kufanya kazi vizuri, maishani mwake.
Mtu huyo hufanana na wale nyuki walioivisha asali nyingi, kwa sababu naye huyajali kwa kuyatunza vizuri mashamba yake mpaka anapata mavuno mengi, katika utekelezaji wa majukumu yake hayo. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “nyuki hawa wana asali.”
Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuzijali kwa kuzitekeleza vizuri kazi zao mpaka wapate mali nyingi, ili waweze kuziendeleza vizuri familia zao, maishani mwao.
Yohana 15:1-2.
Yoshua Bin Sira 11:3.