1127. KALAGU – KIZE. NDITO ALIYO ADIMANILE IGIKI NDITO – JIGANGA.

Ikalagu yiniyo ilolile lijiganga liduma ilo libadikile nulu lyimilile. Iliwe linilo ligikalaga haho pye amakanza bho nduhu ugwimana ilyoyi igiki lililidito. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga giki “ndito aliyo adimanile igiki ndito – jiganga.”

Ikalagu yiniyo, igalenganijiyagwa kuli munhu nshiganu uyo alina wimo wiza umukikalile kakwe. Umunhu ung’winuyo agayombaga mihayo ya nhana na adiko gulenva lulu gugaluchiwa na munhu ungi, kunguno ya bhutungilija bhokwe. Uweyi agabhalangaga abhanhu bhaha kaya yakwe shimile sha gudimila nhungwa ja wiza kunguno ya bhushiganu bhokwe bhunubho, umuwikaji bhokwe.

Umunhu ng’wunuyo agikolaga nili jiganga ilo lidazegejiyagwa kunguno nuweyi alinshiganu umushimilile shakwe pye amakanza, umukikalile kakwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “ndito aliyo adimanile igiki ndito – jiganga.”

Ikalagu yiniyo, yalanga bhanhu higulya ya gubhiza na shimile jishikanu ija gwikala munhungwa jawiza bhuli makanza, kugiki bhadule kujilanhana chiza ikaya jabho, umuwikaji bhobho.

1Petro 2:3-4.

1Petro 2:8.

1Wathesalonike 4:1-2.

 

KISWAHILI: KITENDAWILI  –  TEGA.

MZITO LAKINI HAJITAMBUI KWAMBA NZITO –  MWAMBA.

Kitendawili hicho huangalia mwamba ambao umepachikwa au umesimama. Mwamba huo upo pale ulipo wakati wote na haujitambui kuwa ni mzito. Ndiyo maana watu huhadithiana kwamba, “mzito lakini hajitambui kwamba mzito – Mwamba.”

Kitendawili hicho, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ana msimamo mzuri katika maisha yake. Mtu huyo, huongea maneno ya hekima na ya kweli bila kudanganywa wala kugeuzwa na mtu mwingine kwa sababu ya uaminifu wake. Yeye huwafundisha watu walioko kwenye familia yake namna ya kuwa na msimamo wa kuishi katika maadili mema kwa sababu ya kupenda ukweli kwake, maishani mwake.

Mtu huyo, hufanana na ule mwamba usiosogezwa kwa sababu naye ana msimamo wa kuishi katika maadili mema muda wote katika maisha yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “mzito lakini hajitambui kwamba mzito – Mwamba.”

Kitendawili hicho, hufundisha watu juu ya kuwa na msimamo wa kuishi katika maadili mema siku zote, ili waweze kuzilea familia zao katika maadili hayo mema siku zote, maishani mwao.

1Petro 2:3 – 4.

1Petro 2:8.

1Wathesalonike 4:1-2.

stones-7307274__480

mountains-7427724__480

ENGLISH: I HAVE A RIDDLE – LET IT COME.

HE IS HEAVY BUT HE DOES NOT REALIZE THAT HE IS HEAVY – ROCK.

This puzzle looks at the rock that is embedded or standing. It is there all the time and it does not realize that it is heavy. That is why people tell each other about him that, “he is heavy but he does not realize that he is heavy – Rock.”

This paradox is related to a person who has a good position in his life. Such person, speaks words of wisdom and truth without being deceived or changed by another person because of his honesty. He teaches people in his family on how to have a position of living in good morals because of his love for the truth in his life.

This person is like the unmoved rock because he also has a position of living in good morals all the time in his life. That is why people tell him that, “he is heavy but he does not realize that he is heavy – Rock.”

This riddle imparts in people an idea on having a position of living in good morals all the time, so that they can raise their families in those good morals all the time, in their lives.

1Peter 2:3 – 4.

1 Peter 2:8.

1 Thessalonians 4:1-2.

sharp-2482839__480

Leave a comment

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.