1486. NAMILINGA OSALANG’HANA.

Akahayile kenako kahoyelile munhu uyo agamilinga ng’wiye kunimo gokwe uyo agalema. Umunhu ng’wunuyo agamilinga ung’wiye ng’wunuyo, gung’wambilija gulima ngunda gokwe kunguno goligutale noyi. Uweyi agalima weyi duhu ukungunda gokwe gunuyo kunguno uyo agamilinga gwiza gung’wambilija agalema. Hunagwene aho bhamuja abhiye ung’winikili ngunda agayomba giki, “namilinga osalang’hana.”

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo adina bhumo bho gulungana na bhiye umukikalile kakwe kenako. Umunhu ng’wunuyo, agikalaga bhung’wene bho nduhu ugwiyambilija na bhiye ugutumama imilimo yakwe yiniyo, kunguno ya gugayiwa bhumo bhokwe bhunubho ubho gwiyambilija gutumama milimo nabhiye bhenabho, umuwikaji bhokwe bhunubho. Uweyi agadumaga uguyilela chiza ikaya yakwe yiniyo, kunguno ya nhungwa jakwe jinijo ija gugayiwa bhumo nabhiye bhunubho, umukikalile kakwe kenako.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agabhilingwa gujung’wambilija ng’wiye gujulima ngunda ulema, kunguno nuweyi adina bhumo ubho gwiyambilija nabhiye ugutumama imilimo, umuwikaji bhokwe bhunubho. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “namilinga osalang’hana.”

Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya gubhiza na bhumo bho gwiyambilija gutumama milimo yabho chiza, kugiki bhadule gujibheja chiza ikaya jabho umuwikaji bhobho bhunubho.

Mathayo 22:1-3.

2Petro 1:3.

Waefeso 5:9.

Mathayo 21:28-31.

 

KISWAHILI: NIMEMWALIKA AKAKATAA.

Msemo huo huongelea mtu aliyemwalika mwenzake kumsaidia kwenye kazi yake akakataa. Mtu huyo, alimwalika mwenzake huyo kwenda kumsaidia kulima shamba lake kwa sababu lilikuwa kubwa sana. Yeye alilima yeye tu kwenye shamba lake hilo kwa sababu yule aliyemwalika kuja kumsaidia alikataa. Ndiyo maana watu walimuuliza juu ya yule aliyekataa alisema kwamba, “nimemwalika akakataa.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hana ushirikiano wa kusaidiana na wenzake katika kuyatekeleza majukumu yake, maishani mwake. Mtu huyo huishi peke yake bila ya kusaidiana na wenzake wanaomwalika kuwasaidia kufanya kazi zao, kwa sababu ya kukosa ushirikiano wake na wenzake, katika maisha yake. Yeye hushindwa kuilea vyema familia yake hiyo, kwa sababu ya kukosa ushirikiano wake na wenzake katika utekelezaji wa majukumu yao hayo, maishani mwake.

Mtu huyo, hufanana na yule aliyekataa mwaliko wa kumsaidia mwenzake kulima shamba lake, kwa sababu naye hana ushirikiano wa kusaidiana kufanya kazi na wenzake, maishani mwake. Ndiyo maana watu husema juu yake kwamba, “nimemwalika akakataa.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuwa na ushirikiano wa kusaidiana kufanya kazi na wenzao vizuri, ili waweze kuzilea vyema familia zao, maishani mwao.

Mathayo 22:1-3.

2Petro 1:3.

Waefeso 5:9.

Mathayo 21:28-31.

 

Leave a comment

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.