Imhuli ili ndimu nhale noyi iyo yibhakilile abhana ndimi bhichayo. Indimu yiniyo, nulu igacha idub´ola ukulushigu ulumo duhu, kunguno ya bhutale bhoyo bhunubho. Iyoyi ulu yucha mpaga ishigu jikwile, huna yub’ola lulu. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “lushigu lumo ludab´ojaga Mhuli.”
Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo ali na wiyumilija bho gugamala wangu amakoye gakwe, umuwikaji bhokwe. Umunhu ng’winuyo, agabhutumilaga uwiyumilija bhokwe bhunubho, bho gwikala nzala ulu ogayiyagwa ijiliwa ja gulya ulu ulushugu lunulo, kunguno adadulile ugunanuka bho gukija gulya kulushigu lumo duhu. Uweyi agabhambilijaga na bhiye ugugamala wangu amakoye gabho genayo, kunguno ya wiyumilija bhokwe bhunubho, umuwikaji bhokwe.
Umunhu ng’wunuyo, agikolaga ni Mhuli iyo idabhojiyagwa na lushugu lumo duhu, ulu yachaga, kunguno nuweyi adabhulagagwa ni nikoye lya lushigu lumo duhu, umuwikaji bhokwe. Hunagwene agabhawilaga abhanhu giki, “lushigu lumo lugab’ojaga Mhuli.”
Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na wiyumilija bho gugamala wangu amakoye gabho, kugiki bhadule gwiyambilija ugulishigila ilikanza lya guyeja chiza na bhichabho, umuwikaji bhobho.
Waebrania 6:15.
Yakobo 5:7-8.
2 Petro 3:9.
1 Samweli 28:20.
KISWAHILI: SIKU MOJA HAIOZESHI TEMBO.
Tembo ni mnyama mkubwa kuwapita wanyama wenzake. Mnyama huyo, hata akifa haozi kwa siku moja kwa sababu ya ukubwa wake huo. Yeye akifa huchukua siku nyingi mpaka kuifikia hali hiyo ya kuoza. Ndiyo maana watu husema kwamba, “siku moja haiozeshi tembo.”
Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ana uvumilivu wa kuyamaliza haraka matatizo yake, katika maisha yake. Mtu huyo, huutumia uvumilivu wake huo kila anapokosa chakula siku hiyo, kwa sababu anaelewa kwamba hawezi kufa kwa njaa ya kushinda bila kula kwa siku moja tu. Yeye huwasaidia na wenzake katika kuyawaliza haraka matatizo yao, kwa kuutumia vizuri utumilivu wake huo, maishani mwake.
Mtu huyo, hufanana na Tembo aliyekufa ambaye hawezi kuoza kwa siku moja tu, kwa sababu naye hauliwi na tatizo la siku moja tu, maishani mwake. Ndiyo maana huwaambia watu kwamba, “siku moja haiozeshi tembo.”
Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na uvumilivu wa kuyamaliza kwa haraka matatizo yao, ili waweze kusaidiana kuifikia hali ya kufurahi vizuri, maishani mwao.
Waebrania 6:15. “Naye baada ya kungoja kwa saburi, Abrahamu alipokea kile kilichoahidiwa.”
Yakobo 5:7-8. “Kwa hiyo, ndugu zangu, vumilieni hadi kuja Kwake Bwana. Angalieni jinsi mkulima angojavyo ardhi itoe mavuno yake yaliyo ya thamani na jinsi anavyovumilia kwa ajili ya kupata mvua za kwanza na za mwisho. Ninyi nanyi vumilieni tena simameni imara, kwa sababu kuja kwa Bwana kumekaribia.”
2 Petro 3:9. “Bwana hakawii kuitimiza ahadi Yake kama watu wengine wanavyodhani kukawia, bali Yeye anawavumilia, maana hataki mtu ye yote aangamie, bali kila mmoja afikilie toba.”
1 Samweli 28:20. “Papo hapo Sauli akaanguka chini akajinyoosha, akiwa amejawa na hofu kwa ajili ya maneno ya Samweli. Nguvu zake zikamwishia kwa maana alikuwa hajala cho chote mchana ule wote na usiku.”
ENGLISH: ONE DAY DOES NOT ROT AN ELEPHANT.
Elephants are bigger than other animals. This animal, even if it dies, will not decay in one day because of its size. Such animal takes many days to decay after vanishing. That is why people say that, “one day does not rot an elephant.”
This proverb is equated to a man who has patience enough to solve his troubles in life. This man uses his patience every time when he is hungry, because he understands that he cannot die of starvation without eating within only one day. He helps them and their colleagues to quickly solve their problems, by making good use of his perseverance, in his life.
This man is like a dead Elephant that did not rot in only one day, because he also does die because of suffering from a problem of a single day in his life. That is why he tells people that “one day does not rot an elephant.”
This proverb teaches people on how to be patient enough to quickly solve their problems, so that they can help each other in achieving a happy life in their lives.
Hebrews 6:15. “And so, after he had patiently endured, he obtained the promise.”
James 5: 7-8 “Therefore, my brethren, be patient until the coming of the Lord. See how the farmer waits for the earth to produce its precious harvest and for how long he will wait for the first and the last rains. Be ye also patient; establish your hearts: for the coming of the Lord draweth nigh.
2 Peter 3: 9 “The Lord is not slack concerning His promise, as some men count slackness; but is long suffering to us-ward, not willing that any should perish, but that all should come to repentance.”
1 Samuel 28:20 “At once Saul fell full length on the ground and became very much afraid because of Samuel’s words. His strength failed him because he had not eaten anything all day and all night. ”